Wizara ya Mambo ya Nje ya Pakistan imesema ziara rasmi ya Rais wa Jamhuri ya Kiislamu ya Iran, Masoud Pezeshkian, nchini Pakistan inaonesha azma ya pamoja ya Tehran na Islamabad ya kuimarisha uhusiano wa kihistoria na kitamaduni, pamoja na kuendeleza amani, utulivu na maendeleo endelevu katika eneo.
Iran imetangaza kuwa inajiandaa kwa mazungumzo muhimu ya kimataifa huku ikisisitiza utekelezaji wa makubaliano ya amani, kuzuia hujuma dhidi ya mchakato huo, na kupendekeza mpango mpya wa usimamizi wa Mlango wa Hormuz ndani ya siku 60.