Alhamdulillah, leo idadi na ubora wa vijana wa muumini, waaminifu na wenye shauku katika nchi hii ni kubwa zaidi sana kuliko kipindi cha mwanzo wa Mapinduzi; leo hali ni hivi; haturidhiki, lakini tahadhari iwepo kuhakikisha njia inafuatwa vizuri.
Inaonekana wazi kuwa vyombo vya habari pinzani, hususan mitandao ya Kifarsi inayohusishwa na Wazayuni na Magharibi, kwa makusudi vimeepuka kuzingatia madai halisi ya wafanyabiashara na badala yake vinalenga kuchochea mivutano na machafuko ya kijamii.