Vyombo vya habari vya maadui vimehusika katika kampeni ya upotoshaji dhidi ya Iran kwa kutumia picha za watu wasiokuwa na uhusiano na matukio ya ndani ya nchi hiyo. Hivi karibuni, hata picha ya mwana wa aliyekuwa waziri mkuu wa Kizayuni, Naftali Bennett, iliwasilishwa kimakosa kama mmoja wa waandamanaji waliodaiwa kuuawa, lengo likiwa ni kupotosha umma wa dunia na kuchochea hisia dhidi ya Jamhuri ya Kiislamu ya Iran.
Kiongozi wa chama cha Majlis Ittehad-ul-Muslimeen nchini India, akijibu mzozo ulioibuka kutokana na mabango yenye maandishi “Nampenda Muhammad” katika jimbo la Uttar Pradesh, ameishutumu serikali ya India na viongozi wa eneo hilo kwa kuweka vizuizi vya kibaguzi na vya upendeleo.