Mapinduzi ya Imam Hussein (a.s) hayakuwa vita vya kijeshi pekee; bali yalikuwa vita kamili vya kihabari na kisaikolojia vilivyolenga nyoyo na akili za watu. Kuanzia mahubiri ya Makka hadi ujumbe ulioandikwa kwa damu huko Karbala, Imam Hussein (a.s) aliwezaje kuhamasisha maoni ya umma dhidi ya utawala wa Yazid? Uchambuzi wa mkakati wa mawasiliano wa Imam (a.s) katika mojawapo ya nyakati nyeti zaidi katika historia ya Kishia, unaonesha mfano wa kipekee wa uanaharakati wa kihabari unaosimama juu ya ukweli.