kiusalama
-
Hilali Nyekundu: Hakuna Majeruhi Walioripotiwa Katika Hafla ya Kuaga Kiongozi Shahidi Licha ya Mamilioni ya Waombolezaji Kushiriki
Shirika la Hilali Nyekundu limetangaza kuwa hadi sasa hakuna majeruhi walioripotiwa katika hafla ya kuaga Kiongozi Shahidi Ayatullah Sayyid Ali Khamenei, licha ya mamilioni ya waombolezaji kushiriki. Shirika hilo limeeleza kuwa mafanikio hayo yametokana na usimamizi mzuri wa tukio hilo pamoja na ushirikiano wa wananchi.
-
Waziri wa Mambo ya Nje wa Iraq: Baghdad Ina Uhusiano Bora Sana na Tehran na Iko Tayari Kusaidia Kumaliza Vita
Waziri wa Mambo ya Nje wa Iraq, Fuad Hussein, amesema kuwa Iraq ina uhusiano mzuri na Iran na Marekani, huku akisisitiza kuwa Baghdad iko tayari kushirikiana na pande zote mbili ili kumaliza vita na kuimarisha amani katika eneo hilo.
-
Jarida la The Economist; limetumia kichwa cha Habari Kikisema: “Hatima ya Kennedy inamsubiri Trump!"
Jarida la The Economist limetoa onyo la kisiasa likirejelea hatima ya John F. Kennedy, likidokeza kuwa mazingira ya mvutano na migawanyiko mikali yanaweza kuongeza hatari za kiusalama kwa Donald Trump.
-
Mtaalamu wa Kituruki katika mazungumzo na ABNA:
“Ukanda wa vizuizi wa Israel dhidi ya Uturuki kupitia makubaliano ya pande tatu Mediterania / Siku ngumu za kiuchumi kwa Uturuki zinakuja”
Ali Haidari, mtaalamu wa masuala ya Uturuki, amesema katika mazungumzo na ABNA kuwa Israel inajaribu kuunda ukanda wa vizuizi dhidi ya Uturuki ili kuizuia kuwasiliana na Afrika na Ulaya kupitia magharibi mwa Uturuki, na pia kuzuia Ankara kunufaika na rasilimali kubwa za Mediterania.
-
Qalibaf: Pakistan ni rafiki wa kweli katika nyakati zote
Spika wa Bunge la Iran ameandika kwenye ukurasa wake binafsi katika mitandao ya kijamii kuwa:“Kwa mwaliko maalumu wa Mheshimiwa Spika wa Bunge la Kitaifa la Pakistan, nimeelekea nchini humo. Kuimarisha uhusiano wa pande mbili kati ya mataifa haya mawili ndugu - hususan katika nyanja za ushirikiano wa kiuchumi na kiusalama - kutakuwa ndiyo mhimili mkuu wa ziara hii.”
-
Magaidi 10, Wakiwemo Wanawake Wawili, Watekwa na Shirika la Taarifa za Kijajusi la Kijeshi la Iraq
Shirika la Taarifa za Kijeshi la Iraq leo limetangaza kuwa katika operesheni mbalimbali za kiusalama, limefanikiwa kuchukua watu 10 wa kigaidi katika maeneo mbalimbali ya nchi, wakiwemo wanawake 2.