Kwa mujibu wa ripoti ya Politico, Marekani inajizuia kuchukua hatua ya kijeshi dhidi ya Iran kutokana na hofu ya kupungua kwa akiba ya silaha na uwezekano wa wanajeshi wake kuuawa au kujeruhiwa, huku mazungumzo yasiyo ya moja kwa moja yakiendelea mjini Geneva kwa upatanishi wa Oman.
Washington Post imetahadharisha katika ripoti yake kwamba Ulaya inakabiliwa na janga la idadi ya watu; janga hili linaweza kuathiri nguvu kazi, ukuaji wa uchumi, na uthabiti wa kijamii wa bara hilo.