Kwa mujibu wa uchambuzi wa Middle East Eye, Iran si kama Venezuela katika muktadha wa migogoro ya kikanda, bali ina “kadi nyingi za kucheza” ambazo zinaweza kuwa na athari kubwa za uharibifu dhidi ya adui zake ikiwa mashinikizo ya kijeshi yanazidi kuongezeka. Ripoti inabainisha kwamba Iran inaweza kulenga vituo vya kijeshi vya Marekani katika eneo la Ghuba, ina uwezo wa kutumia nafasi yake katika Strait of Hormuz kama nguvu ya kisiasa au kijeshi, na pia inaweza kufanya mashambulizi yenye nguvu zaidi dhidi ya Israel ikiwa mzozo utazidi kukua