Katika ujumbe wake kwa mnasaba wa msimu wa Hijja ya mwaka 1447 Hijria, Ayatollah Sayyid Mojtaba Hosseini Khamenei amesisitiza kuwa kauli ya “Allahu Akbar” imekuwa silaha ya msingi ya Umma wa Kiislamu katika kupambana na dhulma na ubeberu. Ameeleza kuwa uamsho wa Kiislamu utaendelea kuenea duniani kupitia mshikamano wa Waislamu, huku akisisitiza umuhimu wa kujitenga na Marekani pamoja na utawala wa Kizayuni katika nyanja za kisiasa na kijamii.