Katika khutba yake, Sheikh Ja'far Mwazoa alieleza kwa ufafanuzi wa kina fadhila zake nyingi, akibainisha namna ambavyo Bibi Fatima (sa) ni kigezo bora cha kuigwa na wanawake wote wa Kiislamu, na hata wanaume wa Umma wa Mtume Muhammad (saww), kutokana na uchamungu wake, hekima yake, na msimamo wake thabiti katika kutetea ukweli.
Majina haya ya heshima (Lakabu) hayakuwa tu kwa lengo la kuitana (ili mradi kuitana, pasina kuwepo kigezo chochote cha msingi), bali yalibeba taarifa za kiroho, madhumuni ya uongozi wa ki_Mungu, na mafunzo kwa Waislamu wote. Kujifunza kuhusu laqabu za Imamu Ridha (a.s) ni kujifunza kuhusu maisha na tabia bora za Kiislamu.