Sudan kwa mwaka wa tatu mfululizo imeorodheshwa juu kabisa katika orodha ya migogoro ya kibinadamu duniani.Nchi nyingine zilizoorodheshwa katika ripoti hiyo ni pamoja na: Myanmar, Jamhuri ya Kidemokrasia ya Kongo, Mali, Burkina Faso, Lebanon, Afghanistan, Cameroon, Chad, Colombia, Niger, Nigeria, Somalia, Syria, Ukraine na Yemen.
Serikali ya Bahrain imezidisha tena juhudi zake za kiusalama, kuanzisha wimbi jipya la ukandamizaji, kuwakamata na kuweka vizuizi vikali dhidi ya wapinzani, wanaharakati na hata wananchi wa kawaida; mkakati ambao umekuwa msingi wa kuendelea kwa utawala huu kwa miaka mingi.