Katika Mwezi Mtukufu wa Ramadhani, ambao ni karamu ya Mwenyezi Mungu, “brand” ya kweli si mavazi ya gharama bali ni taqwa, ikhlasi, subira na maadili mema. Hivi ndivyo vinavyomfanya mja awe mrembo mbele ya Mwenyezi Mungu na kufuzu katika meza ya rehema na maghfira.
"Katika ugeni hakuna hofu ya upweke; marafiki wapendwa wako wengi zaidi upande ule mwingine.”
Kwa maana kwamba: Shahidi anapovuka kutoka dunia hii, haogopi kutengwa, kwa sababu anatambua wazi kuwa upande wa pili kuna kundi kubwa la wacha-Mungu, wakweli, watu wema, na mashahidi waliomtangulia, walio tayari kumpokea katika safu yao.