Kamanda wa Makao Makuu ya Kati ya Khatam al-Anbiya (s.a.w), Jenerali Ali Abdullahi, ameonya nchi za eneo hilo dhidi ya kutegemea Marekani kwa ulinzi, akisema utegemezi huo unaweza kuzifanya kuwa sehemu ya migogoro na vita.
Hadhramout, jimbo kubwa na lenye utajiri mkubwa zaidi nchini Yemen, limeingia rasmi kwenye udhibiti wa Baraza la Mpito la Kusini (STC) baada ya kusonga mbele kwa kasi kwa vikosi vyake. Hatua hii imeufanya mkoa huo kuwa uwanja muhimu wa kuchorwa upya kwa ramani ya madaraka mashariki mwa Yemen.