Katibu Mkuu wa Hezbollah amesema kuwa mpango wa kuangamiza Iran na muqawama umefeli, akisisitiza kuwa kusitishwa kwa mapigano lazima kuwe kwa masharti ya kusitishwa kabisa kwa uvamizi na kujiondoa kwa adui katika maeneo wanayoyakalia.
Mwenyekiti wa Baraza la Wanazuoni wa Kiislamu wa Bahrain alisisitiza kuwa kuacha njia ya Muqawama (mapambano dhidi ya wavamizi na dhulma) hakuzai chochote isipokuwa fedheha, udhalilishaji na utumwa.
Ayatollah Khamenei katika kikao na Rais pamoja na Baraza la Mawaziri alisisitiza juu ya umuhimu wa 'kutawala kwa hali ya kazi, juhudi na matumaini' dhidi ya 'hali ya si vita wala amani'