Waziri wa Mambo ya Nje wa Iran, Abbas Araghchi, amesema ujumbe wa hivi karibuni wa Kiongozi wa Mapinduzi ya Kiislamu ni mwongozo muhimu kwa maafisa wote wa sera za nje na utasaidia kulinda heshima ya taifa pamoja na haki za wananchi wa Iran.
Hujjatul-Islam wal-Muslimin Babakhani pia alisisitiza nafasi ya wanawake katika hay’a na kusema: “Tangu kuundwa kwa hay’a, wanawake wamekuwa mstari wa mbele katika uongozi wa kitamaduni na kidini - kuanzia Bibi Fatima az-Zahra (a.s) na Bibi Zaynab (a.s) hadi leo - na wametoa mchango mkubwa katika kuhifadhi na kueneza utamaduni wa hay’a. Uwepo wao umeleta athari kubwa katika kufundisha mafundisho ya dini na kuonyesha kwa jamii fadhila za Ahlul-Bayt (a.s).”