Hujjatul-Islam wal-Muslimin Babakhani pia alisisitiza nafasi ya wanawake katika hay’a na kusema: “Tangu kuundwa kwa hay’a, wanawake wamekuwa mstari wa mbele katika uongozi wa kitamaduni na kidini - kuanzia Bibi Fatima az-Zahra (a.s) na Bibi Zaynab (a.s) hadi leo - na wametoa mchango mkubwa katika kuhifadhi na kueneza utamaduni wa hay’a. Uwepo wao umeleta athari kubwa katika kufundisha mafundisho ya dini na kuonyesha kwa jamii fadhila za Ahlul-Bayt (a.s).”