Maelfu ya waumini wa Ahlul-Bayt (as) jijini Dar es Salaam wamefanya Masira ya A'shura katika Wilaya ya Temeke kwa lengo la kuhuisha ujumbe wa Imam Hussein (as), kulaani mauaji ya Karbala na kusisitiza kusimama upande wa haki, uadilifu na kupinga dhulma.
Baada ya mashambulizi makubwa ya vyombo vya habari vya Uingereza dhidi ya mbio ya hisani iliyoandaliwa na Msikiti wa East London kwa sababu ya utenganishaji wa kijinsia, Tume ya Usawa na Haki za Kibinadamu ya Uingereza imeitangaza kwamba waandaaji wa tukio hilo wamekubali kupitia upya sera zake kabla ya awamu ijayo ya mashindano.
Hata hivyo, msikiti huo umeeleza kwamba matukio kama hayo yapo kwa wingi katika maeneo mbalimbali ya Uingereza-ikiwemo mashindano maalumu ya wanawake na vipindi vya kuogelea vinavyoandaliwa katika vituo vya jamii ya Kiyahudi-lakini hakuna hata moja kati ya matukio hayo yaliyowahi kusababisha mjadala au msukosuko kama huu.