Kwa mujibu wa ripoti ya Shirika la Habari la Ahlul-Bayt (a.s.) – ABNA – viongozi wa Chama cha Congress cha India Jumatano, kabla ya Modi kuondoka kwenda Palestina inayokaliwa, walisisitiza kwamba wakati nchi nyingi na maoni ya umma duniani yanaishutumu sera ya Netanyahu kwa vita vyake vya uharibifu dhidi ya Gaza na upanuzi wa makazi haramu katika Ukingo wa Magharibi, Waziri Mkuu wa India anaonesha aina ya "kushirikiana kwa aibu" na Tel Aviv.
Modi amesafiri kwa ziara ya siku mbili kwenda Palestina inayokaliwa na mbali na kukutana na Netanyahu, amepanga kuhutubu katika bunge la utawala wa Kizayuni (Knesset) pia; hatua ambayo kwa mujibu wa wakosoaji, katika kilele cha kuongezeka kwa ukatili dhidi ya raia Wapalestina, itatuma ujumbe wazi wa kisiasa wa kuunga mkono serikali kali ya Israel.
Katika muktadha huo, Jiram Ramesh, Katibu Mkuu wa Chama cha Congress, katika ujumbe wake kwenye mtandao wa kijamii wa X (ulioitwa zamani Twitter), kwa kukumbusha historia ya India katika kuunga mkono Palestina aliandika: Mnamo Mei 20, 1960, Jawaharlal Nehru alihudhuria Gaza na kukutana na vikosi vya India vilivyokuwa vimewekwa ndani ya mfumo wa Kikosi cha Dharura cha Umoja wa Mataifa. Pia mnamo Novemba 29, 1981, India ilitoa stempu ya kumbukumbu kwa mshikamano na Palestina na mnamo Novemba 18, 1988 pia iliitambua nchi ya Palestina.
Congress ya Kitaifa ya India: Safari ya Modi kwa Israel ni "Uwoga wa Kimaadili" dhidi ya ukatili wa Gaza
Ramesh alibainisha: "Kipindi kile kilikuwa zama nyingine. Leo hii lakini Waziri Mkuu wa India anamkumbatia waziwazi Waziri Mkuu wa Israel; mtu ambaye ameigeuza Gaza kuwa lundo la mavumbi na magofu na wakati huo huo anaendeleza upanuzi wa makazi haramu katika Ukingo wa Magharibi uliokaliwa." Aliongeza kwamba wakati Netanyahu hata ndani ya ardhi zilizokaliwa anakabiliwa na maandamano makubwa na mashtaka mazito ya ufisadi, Modi kwa safari hii anaonesha "uwoga wa kimaadili."
Kiongozi huyu wa Congress pia kwa kurejelea kuongezeka kwa mchakato wa kunyang'anywa ardhi na kukimbizwa kwa maelfu ya Wapalestina katika Ukingo wa Magharibi uliokaliwa, alizitaja hatua hizi kuwa ni mfano wa sera za kimfumo za uhamisho wa kulazimishwa zinazokabiliwa na lawama kubwa ya kimataifa. Kwa mujibu wake, mashambulio ya utawala wa Kizayuni dhidi ya raia huko Gaza yanaendelea bila kukoma na wakati huo huo ripoti zimechapishwa kuhusu mipango ya pamoja ya Marekani na Israeli ya mashambulio ya anga dhidi ya Iran.
Ramesh akiendelea kwa kukosoa kile alichokielezea kama "mahusiano maalum na yasiyo wazi" kati ya serikali ya Modi na duru za Kizayuni, alisema: "Serikali ya Modi imechukua mkabala wa uwili na unao na unafiki kwa kutoa matamshi yanayoonekana kuunga mkono dhamira ya Palestina, wakati ukweli wa nyanjani unaonyesha kwamba New Delhi kwa vitendo umejiondoa kutoka misimamo yake ya kihistoria."
Alisisitiza kwamba India ilikuwa miongoni mwa nchi za kwanza zilizoitambua nchi ya Palestina mwaka 1988 na daima ilitetea haki za watu wa Palestina katika mabaraza ya kimataifa; lakini sasa, urithi huu wa kihistoria unadhoofishwa katika kivuli cha ukaribu wa kimkakati na Tel Aviv.
Safari ya Modi kwenye ardhi zilizokaliwa inafanyika wakati utawala wa Kizayuni unakabiliana na migogoro ya ndani, maandamano dhidi ya kudhoofisha uhuru wa mamlaka ya mahakama na kesi za ufisadi za Netanyahu. Baadhi ya ripoti zinaonyesha kuwa sehemu ya misimamo ya upinzani katika ardhi zilizokaliwa pia imetishia kususia hotuba ya Waziri Mkuu wa India katika Knesset kwa kupinga sera za Netanyahu.
Kwa jumla, Chama cha Congress kinaitathmini safari hii si tu kama hatua ya kidiplomasia, bali kama ishara ya mageuzi ya kimkakati katika sera ya kigeni ya India na kinaielezea kama kukaidi mila ya muda mrefu ya kuunga mkono watu wa Palestina na dhamira ya haki; msimamo ambao kwa maoni ya chama hiki, utakuwa na matokeo mapana ya kimaadili na kisiasa kwa nafasi ya kimataifa ya New Delhi.
Your Comment