Maulid hayo yamehitimishwa kwa dua maalum ya kuombea umoja wa Waislamu, amani ya taifa na ustawi wa jamii, sambamba na pongezi kwa waandaaji wote waliowezesha kufanyika kwa hafla hiyo kwa mafanikio makubwa.
Mufti Mkuu alitoa wito maalum kwa wanasiasa na wananchi wote katika kipindi hiki cha kuelekea uchaguzi, kuendelea kulinda amani, kuepuka maneno ya chuki na kuhakikisha Tanzania inabaki kuwa nchi ya utulivu na maridhiano.