Akaongeza kuwa “Kitengo kimeandaa vituo viwili vya kutolea huduma za afya, kituo kimoja cha wanaume na kingine cha wanawake”, akasema: “Huduma zinazotolewa zinahusisha huduma za dharura, kupima sukari, damu na kutoa dawa kulingana na hali ya mgonjwa”.
Akafafanua kuwa “Jopo la madaktari linaudwa na madaktari wa kike 14 na wanaume 35, wamekuja kutoka kwenye vituo vya afya vya mikoa tofauti, Diwaniyya, Hilla, Naswiriyya, Karbala. Wametoa huduma za matibabu, kinga pamoja na maelekezo ya afya”.