Abbas Araqchi
-
Waziri wa Mambo ya Nje wa Iran amesema makubaliano na Marekani yako “karibu kufikiwa”; Trump asema anapendelea diplomasia
Abbas Araghchi amesema makubaliano na Marekani yako karibu kufikiwa ikiwa diplomasia itapewa kipaumbele, huku Donald Trump akisisitiza kuwa anapendelea mazungumzo badala ya vita.
-
Abbas Araghchi: Makubaliano Yanawezekana Ikiwa Diplomasia Itapewa Kipaumbele
Abbas Araghchi amesema kuwa mazungumzo kati ya Iran na Marekani yataanza tena mjini Geneva kwa kuzingatia makubaliano ya awali, akisisitiza kuwa Tehran ina nia ya dhati ya kufikia makubaliano ya haki haraka iwezekanavyo. Ameeleza kuwa Iran haitafuti silaha za nyuklia, lakini haitakubali kunyimwa haki yake ya kutumia teknolojia ya nyuklia kwa malengo ya amani, akibainisha kuwa huu ni “wakati wa kihistoria” wa kutatua wasiwasi wa pande zote kupitia diplomasia.
-
Abbas Araghchi: Makubaliano yako karibu iwapo diplomasia itapewa kipaumbele
Abbas Araghchi amesema kuwa makubaliano kati ya Iran na Marekani yako ndani ya mfukoni iwapo diplomasia itapewa kipaumbele, akisisitiza kuwa Iran haitafuti silaha za nyuklia lakini haitarudi nyuma katika haki yake ya teknolojia ya amani ya nyuklia.
-
Mchezo wa Subira na Mizania; The Guardian yaangazia mtindo wa mazungumzo wa Abbas Araghchi kuelekea mazungumzo ya nyuklia
Uchambuzi wa The Guardian unaeleza kuwa Abbas Araghchi anatumia mkakati wa subira na mizania katika mazungumzo ya nyuklia, huku ukilinganisha diplomasia ya Iran na mchezo wa chess na ile ya Donald Trump na mieleka, na kubainisha kuwa mafanikio yatategemea hatua za pamoja zisizoweza kubadilishwa.
-
Araghchi na Takht-Ravanchi Wakagua Nyaraka Muhimu Kabla ya Mazungumzo ya Nyuklia Iran–Marekani Muscat
Waziri wa Mambo ya Nje wa Iran, Seyyed Abbas Araghchi, pamoja na Naibu wake Majid Takht-Ravanchi, wameonekana wakipitia nyaraka muhimu kabla ya kuanza kwa mazungumzo ya nyuklia kati ya Iran na Marekani mjini Muscat, Oman.
-
Waziri wa Mambo ya Nje wa Iran Abbas Araghchi Aongoza Ujumbe wa Mazungumzo na Marekani Muscat
Waziri wa Mambo ya Nje wa Iran, Abbas Araghchi, ameongozana na ujumbe wake wa kidiplomasia kuelekea mjini Muscat, Oman, kwa ajili ya mazungumzo na Marekani. Mazungumzo hayo yanatazamwa kuwa na umuhimu mkubwa katika kujadili masuala ya nyuklia, vikwazo vya kiuchumi na usalama wa kikanda, kwa lengo la kufungua ukurasa mpya wa maelewano ya kisiasa.
-
Waziri wa Mambo ya Nje wa Iran Akutana na Naibu Mkuu wa Baraza Kuu la Kishia Lebanon Beirut
Wakati wa ziara yake rasmi mjini Beirut, Waziri wa Mambo ya Nje wa Iran, Seyyed Abbas Araghchi, alikutana na Sheikh Ali Al-Khatib, Naibu Mkuu wa Baraza Kuu la Kiislamu la Kishia nchini Lebanon. Mazungumzo yao yalijikita katika maendeleo ya kikanda, umuhimu wa umoja wa Kiislamu, na kuimarisha ushirikiano wa kidini na kisiasa kwa ajili ya uthabiti na mshikamano wa Lebanon.
-
Araqchi: Marekani Haitaki Diplomasia ya Kweli, Bali Kulazimisha Iran Kunyimwa Haki Zake
Araqchi: "Diplomasia ya kweli haiwezi kujengwa juu ya mashinikizo na masharti ya upande mmoja. Kuitaka Iran iachane na haki zake halali si mazungumzo, bali ni jaribio la kulazimisha,”
-
Iran yashuku ujumbe wa Netanyahu kuhusu kutoshambulia tena
"Vikosi vya ulinzi vya Iran vipo katika hali ya tahadhari ya juu kwa sababu kuna uwezekano mkubwa wa hila kutoka Israel, na hatuamini nia hizi".
-
Iran: Hatuna Imani na Israel Kuheshimu Usitishaji Mapigano Gaza / Mkataba wa Amani wa Abraham ni Usaliti Mkubwa – Araghchi
“Kila mara Israel inaposhindwa kijeshi au inapokabiliwa na shinikizo la kimataifa, hukubali makubaliano ya muda tu ili kupata nafasi ya kujipanga upya na kuendeleza mashambulizi mapya. Hivyo, amani ya kweli haiwezi kupatikana kwa kutegemea ahadi zake.”
-
Waziri wa Mambo ya Nje wa Iran:
"Kila afisa wa Kijeshi au Mwanasayansi wa Nyuklia wa Iran anayeuliwa Kigaidi, kuna wengine mia moja nyuma yake walioko tayari kuchukua nafasi yake"
Abbas Araqchi alisema: "Tofauti na utawala wa Kizayuni, Iran haitaficha kamwe hasara zake na inajivunia Mashahidi wake kama vielelezo vya ujasiri. Taifa la Iran litasimama kidete dhidi ya yeyote anayejaribu kuliamulia mustakabali wake hadi tone la mwisho la damu".