Abbas Araqchi
-
Waziri wa Mambo ya Nje wa Iran Akutana na Naibu Mkuu wa Baraza Kuu la Kishia Lebanon Beirut
Wakati wa ziara yake rasmi mjini Beirut, Waziri wa Mambo ya Nje wa Iran, Seyyed Abbas Araghchi, alikutana na Sheikh Ali Al-Khatib, Naibu Mkuu wa Baraza Kuu la Kiislamu la Kishia nchini Lebanon. Mazungumzo yao yalijikita katika maendeleo ya kikanda, umuhimu wa umoja wa Kiislamu, na kuimarisha ushirikiano wa kidini na kisiasa kwa ajili ya uthabiti na mshikamano wa Lebanon.
-
Araqchi: Marekani Haitaki Diplomasia ya Kweli, Bali Kulazimisha Iran Kunyimwa Haki Zake
Araqchi: "Diplomasia ya kweli haiwezi kujengwa juu ya mashinikizo na masharti ya upande mmoja. Kuitaka Iran iachane na haki zake halali si mazungumzo, bali ni jaribio la kulazimisha,”
-
Iran yashuku ujumbe wa Netanyahu kuhusu kutoshambulia tena
"Vikosi vya ulinzi vya Iran vipo katika hali ya tahadhari ya juu kwa sababu kuna uwezekano mkubwa wa hila kutoka Israel, na hatuamini nia hizi".
-
Iran: Hatuna Imani na Israel Kuheshimu Usitishaji Mapigano Gaza / Mkataba wa Amani wa Abraham ni Usaliti Mkubwa – Araghchi
“Kila mara Israel inaposhindwa kijeshi au inapokabiliwa na shinikizo la kimataifa, hukubali makubaliano ya muda tu ili kupata nafasi ya kujipanga upya na kuendeleza mashambulizi mapya. Hivyo, amani ya kweli haiwezi kupatikana kwa kutegemea ahadi zake.”
-
Waziri wa Mambo ya Nje wa Iran:
"Kila afisa wa Kijeshi au Mwanasayansi wa Nyuklia wa Iran anayeuliwa Kigaidi, kuna wengine mia moja nyuma yake walioko tayari kuchukua nafasi yake"
Abbas Araqchi alisema: "Tofauti na utawala wa Kizayuni, Iran haitaficha kamwe hasara zake na inajivunia Mashahidi wake kama vielelezo vya ujasiri. Taifa la Iran litasimama kidete dhidi ya yeyote anayejaribu kuliamulia mustakabali wake hadi tone la mwisho la damu".