Kwa mujibu wa taarifa hiyo, matukio kadhaa ya amani ya kidini yaliyoandaliwa na Harakati ya Kiislamu ya Nigeria chini ya uongozi wa Sheikh Zakzaky, likiwemo Kongamano la Mwaka la Mauaji ya Zaria ya mwaka 2015 na programu ya Nisfu / Nusu Sha’ban kwa ajili ya kuadhimisha Maulid ya Imam Mahdi (a.t.f.s), yaliripotiwa kuvurugwa na vikosi vya usalama.
Makumi ya waandamanaji wanaounga mkono Palestina wameuawa na kujeruhiwa baada ya vikosi vya usalama kuwafyatulia risasi wakiwa kwenye Maandamano ya Siku ya Kimataifa ya Quds katika Mji Mkuu wa Nigeria.