Bibi Ummul-Baneen aliwapenda Ahlul-Bayt wa Mtume kuliko alivyowapenda wanawe mwenyewe. Alipopata habari za huzuni za Karbala, hakumuuliza kwanza kuhusu wanawe wanne, bali alisema:
“Nijulisheni kuhusu Hussein.”
Uharibifu wa Jannat al-Baqii umeacha doa lisilofutika katika historia ya Uislamu. Makaburi haya hayakuwa tu sehemu ya kumbukumbu ya kihistoria, bali pia yalikuwa alama ya mapenzi na heshima kwa watu waliotumikia Uislamu kwa ikhlasi na kujitolea.
Leo hii, Waislamu kote duniani wanaendelea kuomba urejesheaji Heshima na Staha inayostahili kwa Makaburi haya matukufu.