Uharibifu wa Jannat al-Baqii umeacha doa lisilofutika katika historia ya Uislamu. Makaburi haya hayakuwa tu sehemu ya kumbukumbu ya kihistoria, bali pia yalikuwa alama ya mapenzi na heshima kwa watu waliotumikia Uislamu kwa ikhlasi na kujitolea.
Leo hii, Waislamu kote duniani wanaendelea kuomba urejesheaji Heshima na Staha inayostahili kwa Makaburi haya matukufu.
Mnamo mwaka wa 1220 A.H., Mawahabi waliutwaa mji huo baada ya kuzingirwa kwa mwaka mmoja na nusu na kwa sababu ya njaa huko Madina. [25] Kulingana na vyanzo vilivyopo, baada ya kujisalimisha kwa Madina, Saud bin Abdul Aziz alitaifisha mali yote iliyokuwa kwenye hazina ya Madhabahu ya Mtume na pia akaamuru kuharibiwa kwa majengo na majumba yote ya Madina, pamoja na makaburi ya Baqi.[26]