Sudan kwa mwaka wa tatu mfululizo imeorodheshwa juu kabisa katika orodha ya migogoro ya kibinadamu duniani.Nchi nyingine zilizoorodheshwa katika ripoti hiyo ni pamoja na: Myanmar, Jamhuri ya Kidemokrasia ya Kongo, Mali, Burkina Faso, Lebanon, Afghanistan, Cameroon, Chad, Colombia, Niger, Nigeria, Somalia, Syria, Ukraine na Yemen.
Burkina Faso sasa imeizidi Senegal katika uzalishaji wa vitunguu na kuwa nchi ya tatu kwa uzalishaji mkubwa wa vitunguu katika eneo la Afrika Magharibi.Mafanikio haya yamechangiwa kwa kiasi kikubwa na uongozi bora wa Rais Ibrahim Traoré, ambaye ameweka mkazo katika kuimarisha sekta ya kilimo na kuinua maisha ya wakulima wa kawaida.