Dr. Alhad Mussa Salum ametoa wito kwa Waumini na watu wote wa Dar -es- Salaam na vitongoji vyake kuhudhuria kwa wingi katika hafla hiyo akisisitiza:
“Tumuadhimishe Mtume Muhammad (s.a.w.w), tumtukuze, na tufuate nyayo zake kwa upendo na amani.”
Kwa kutambua mchango huo, JMAT-TAIFA iliishukuru na inaendelea kuishukuru kwa dhati Wizara ya Habari, Utamaduni, Sanaa na Michezo kwa ushirikiano wao madhubuti, na walisisitiza kuwa mshikamano huo utaendelea kwa ajili ya maendeleo na ustawi wa jamii zote za Taifa pendwa la Tanzania