Fiqhi
-
Katibu Mkuu wa Jumuiya ya Kimataifa ya Ahlul-Bayt (a.s): Imam Khomeini (r.a) Aliirejesha Dini Kutoka Pembezoni Hadi Kiini cha Jamii na Utawala
Katibu Mkuu wa Jumuiya ya Kimataifa ya Ahlul-Bayt (a.s), Ayatullah Reza Ramadhani, amesema kuwa Imam Khomeini (r.a) aliirejesha dini kutoka pembezoni hadi kuwa kiini cha maisha ya kijamii na mfumo wa utawala, akithibitisha kuwa dini inaweza kuwa msingi wa uongozi, haki ya kijamii na ujenzi wa ustaarabu wa kisasa.
-
Fiqh ya Kuangalia Baadaye; Njia Pekee ya Kulinda Jamii Dhidi ya Ufisadi wa Akili Bandia
Mwalimu wa Chuo cha Dini cha Qom amesema kwamba akili bandia (AI) imeunda mipaka mipya katika eneo la uwajibikaji, mamlaka, na haki. Aliongeza kuwa: Fiqh inapaswa kuwa na mtazamo wa kuangalia mbele, ili iweze kutoa hukumu na msingi wa dini kwa matukio mapya kabla ya kuibuka kwa migogoro au majanga.
-
Ujumbe wa Kiongozi Mkuu wa Mapinduzi kwa mkutano wa kumbukumbu ya miaka mia moja (100) ya kuanzishwa upya kwa Chuo cha Dini cha Qom:
Ayatollah Khamenei: Jukumu la (Hawza) Chuo cha Kidini ni Kuchora Mipaka Mikuu na Midogo ya Ustaarabu mpya wa Kiislamu
"Kazi kuu na ya msingi ya Hawza ni (البَلاغُ المُبین) kufikisha ujumbe wa dini kwa uwazi na ufasaha (ubalighi wa wazi - Kwa maana: Kufikisha ujumbe kwa uwazi na uthabiti na kwa namna ambayo haiachi shaka yoyote -). Miongoni mwa vielelezo vyake muhimu kabisa ni kuchora na kueleza kwa uwazi mistari (mipaka) mikuu na ya kando ( au midogo) ya ustaarabu mpya wa Kiislamu, pamoja na kuifafanua, kuieneza, na kuikuza katika jamii kama sehemu ya utamaduni."