Naibu Waziri wa Mambo ya Nje wa Iran, Kazem Gharibabadi, amesema Iran haitaruhusu mamlaka yake, umoja wa ardhi wala usalama wa taifa kuwa sehemu ya propaganda au mashinikizo ya kisiasa kutoka kwa Marekani na washirika wake.
Naibu Waziri wa Mambo ya Nje wa Iran, Kazem Gharibabadi, amesema kuwa Iran na Oman ndizo pekee zenye haki ya mamlaka juu ya Mlango-Bahari wa Hormuz, akisisitiza kuwa hakuna nchi nyingine inayopaswa kuingilia usimamizi wa njia hiyo muhimu ya baharini.