Mahakama ya Kimataifa ya Uhalifu (ICC) Jumatatu usiku ilikataa pingamizi la kisheria na ombi la rufaa la utawala wa Kizayuni wa Israel, na hivyo kuweka wazi njia ya kuendelea na uchunguzi wa uhalifu wa kivita unaofanywa na utawala huo katika Ukanda wa Gaza.
Dk. Ali Matar, mhadhiri wa Sayansi ya Siasa na mtafiti wa masuala ya uhusiano wa kimataifa na sheria za kimataifa katika Chuo Kikuu cha Lebanon, amesisitiza kuwa kukiri kwa Donald Trump kuhusu ushiriki wa Marekani katika vita dhidi ya Iran ni ushahidi rasmi wa uvamizi na uvunjaji wa Mkataba wa Umoja wa Mataifa.