Sheikh Saleh Al-Talib mnamo mwaka 2018 katika moja ya khutba zake alipinga maonesho ya muziki (konseti) na mikusanyiko ya kijinsia iliyochanganyika, jambo lililosababisha kutoridhishwa na viongozi wa Saudia na pia shinikizo kutoka kwa taasisi za kiserikali zinazohusiana na Mamlaka Kuu ya Burudani ya Saudi Arabia, na hatimaye kusababisha kukamatwa kwake.
Sheikh Dr.Alhad Mussa Salum amewahimiza Waumini wa Dar es Salaam na maeneo ya jirani kuhudhuria kwa wingi, akisisitiza kuwa mwaka huu Maulid itakuwa na vionjo vya pekee, ikiwa ni kumbukumbu ya kumsifu na kufuata nyayo za Mtume Muhammad (s.a.w).