Indonesia
-
Waziri wa Mambo ya Nje wa Iran Akutana na Mwenzake wa Indonesia mjini Mashhad
Waziri wa Mambo ya Nje wa Iran, Abbas Araghchi, amekutana na Waziri wa Mambo ya Nje wa Indonesia, Sugiono, mjini Mashhad, wakati ujumbe wa ngazi ya juu kutoka Indonesia ukiendelea na ziara ya kutoa rambirambi kufuatia kuuawa shahidi kwa Kiongozi wa Mapinduzi ya Kiislamu.
-
Waziri wa Mambo ya Nje wa Indonesia Awasili Mashhad Kutoa Rambirambi kwa Kiongozi Shahidi wa Mapinduzi ya Kiislamu
Ujumbe wa ngazi ya juu kutoka Indonesia, ukiongozwa na Waziri wa Mambo ya Nje pamoja na viongozi wa kisiasa na wanazuoni wa Kiislamu, umewasili katika mji mtakatifu wa Mashhad kwa ajili ya kutoa pole kufuatia kuuawa shahidi kwa Kiongozi wa Mapinduzi ya Kiislamu.
-
Mazungumzo yaendelea kwa ajili ya kufikia makubaliano ya kunyang’anya silaha Gaza / Kikosi cha Indonesia chatarajiwa kuwasili mwezi Machi
Katika muktadha wa kunyang’anya silaha huko Gaza, mapendekezo mengi yamewasilishwa. Inabakia kuonekana iwapo Hamas na makundi ya muqawama watakubali kikamilifu suala hili. Hapo awali, mazungumzo yalihusu tu silaha nzito, lakini sasa yanajumuisha pia silaha za mtu binafsi.
-
Profesa wa Chuo Kikuu cha Indonesia katika mahojiano na ABNA:
“Iran ni mfano wa kipekee wa maendeleo ya kisayansi na uimara dhidi ya vikwazo – ni lazima mtu aione kwa macho yake”
Amesema kuwa uongo mwingi kuhusu Iran unatolewa na taasisi zinazopingwa na msimamo wa Iran wa kusimama dhidi ya Marekani na Israel. Hata hivyo, baada ya vita vya siku kumi na mbili, wanafikra wengi duniani wamekiri wazi kwamba Iran ndilo taifa pekee lililosimama dhidi ya dhulma kwa njia ya kivitendo, si kwa maneno tu.
-
Katibu Mkuu wa Mtandao wa Uhuru wa Palestina nchini Indonesia (FPN) katika mahojiano na Shirika la Habari la AhlulBayt (ABNA):
"Msaada kwa Palestina unapaswa kuongozwa kwa ufanisi, kuandaliwa kwa umoja na kuongezwa mara kadhaa"
"Ni kweli kwamba usitishaji wa vita umewapa Wapalestina muda wa kupumua, lakini tunapaswa kuwa waangalifu dhidi ya mpango wa kibepari wa Trump. Haiwezekani Marekani - ambayo ni mshirika mkuu katika mauaji ya Wapalestina - kuwa msuluhishi wa haki. Katika mpango wa vipengele 20 wa Trump, hakuna popote palipotajwa uhuru wa Palestina.”