Kwa mujibu wa mtandao wa BBC, ufafanuzi huo umeandaliwa na Kikosi Kazi cha Islamophobia/Chuki dhidi ya Waislamu, na tayari umewasilishwa serikalini, huku sasa ukiwekwa katika mchakato wa mashauriano na wadau mbalimbali. Serikali ya Uingereza iliunda kikosi kazi hicho mwezi Februari mwaka huu, na pendekezo lake la mwisho liliwasilishwa mwezi Oktoba.
Wataalamu: Sheria hizi zinalenga kundi moja tu - Waislamu
Nicolas Cadène, ambaye ni mtaalamu maarufu wa sheria ya Ulaikishe na aliyewahi kuwa ripota wa Kituo cha Uangalizi wa Ulaikishe, ameiambia France 24 kwamba: “Mipango hii inawalenga Waislamu pekee, na inaonyesha kukubalika kwa ubaguzi wa wazi.”