Umoja wa Wanazuoni wa Kiislamu Ulimwenguni umetoa Fat'wa kuhusu Wajibu wa Jihadi katika kuunga mkono Ghaza na kusisitiza kuwa, Jihadi dhidi ya utawala wa Kizayuni na mamluki na askari wake wanaohusika na mauaji ya halaiki ya watu wa Ghaza katika ardhi zinazokaliwa kwa mabavu za Palestina ni wajibu mutlaki (unaomgusa kila mtu).
Katika kizingiti cha Siku ya Quds Duniani, Jumuiya ya Walimu wa Seminari ya Qom imetoa taarifa ikizitaka sehemu zote za Taifa pendwa la Iran kushiriki kikamilifu katika Matembezi ya Amani ya Siku hii ya Quds na kutangaza kwa mara nyingine uungaji mkono wao kwa Muqawamah (Upinzani) wa Kiislamu wa Palestina.