Kampuni ya CinnaGen ya Iran imepata mafanikio makubwa baada ya dawa yake ya Zandoriah (teriparatide) kuidhinishwa kuuzwa katika nchi 27 za Umoja wa Ulaya pamoja na nchi tatu za EEA, hatua inayochukuliwa kuwa mafanikio muhimu kwa sekta ya dawa na teknolojia ya afya ya Iran.
Kampuni ya uchimbaji madini ya Barrick Gold imelipa Faranga za CFA bilioni 275 kwa Serikali ya Mali ikiwa ni sehemu ya fedha zilizokuwa zikidaiwa na mamlaka za nchi hiyo, hatua inayotajwa kuwa matokeo ya msimamo mkali wa Bamako katika kusimamia rasilimali zake za taifa.
Wizara ya Ulinzi ya Israel imetiliana saini mkataba mkubwa na Kampuni ya Rafael ili kuongeza kwa kiasi kikubwa uzalishaji wa makombora ya kukinga ya mfumo wa Iron Dome (Gombo la Chuma).