Ayatullah al-Udhma Sheikh Nasir Makarim Shirazi amesema kuwa waliohusika na mauaji ya Kiongozi Shahidi wa Mapinduzi ya Kiislamu, pamoja na viongozi, raia wasio na hatia na watoto waliouawa, hawataokoka adhabu ya Mwenyezi Mungu na kwamba damu za mashahidi hao hazitasahaulika kamwe.
Nadhami Ardakani ametaja kaulimbiu ya “Mkutano Mkuu wa Nne wa Masadat” kuwa:
"Masadat ni Wabeba Bendera wa Mapambano dhidi ya Utawala wa Kizayuni na Watunzi wa Historia ya Baadaye",
na akasema: Baada ya ushindi wa Mapinduzi ya Kiislamu, bendera ya kupambana na Uzayuni ilipeperushwa kwa mara ya kwanza na Imam Khomeini (r.a), kisha ikakabidhiwa kwa Kiongozi Mkuu wa Mapinduzi ambaye mwenyewe ni katika Masadat, na baadaye ikaendelezwa na watu kama Shahidi Sayyid Hassan Nasrallah, Sayyid Badruddin Houthi na Ayatollah Sistani.