Katika ujumbe wake mzito kwa jumuiya ya kimataifa, Balozi Matinyi alisisitiza kuwa Tanzania ya sasa inatafuta wafanyabiashara na wawekezaji, si wafadhili. Taifa linaendelea kutekeleza miradi mikubwa ya kimkakati ikiwemo Reli ya Kisasa (SGR), pamoja na mradi wa gesi asilia unaokadiriwa kugharimu dola bilioni 42, miradi inayolenga kuimarisha uchumi wa taifa na nafasi yake katika uchumi wa kikanda na kimataifa.
Harakati ya Upinzani ya Kiislamu ya Palestina (Hamas) imesema kuwa haina nia ya kushiriki katika mipango ya utawala wa ukanda wa Gaza baada ya kuisha kwa mashambulizi ya utawala wa kikoloni, na imeitaka kuundwa kwa kamati ya usimamizi kwa makubaliano ya makundi yote ya Kipalestina.