Kikao hiki kimeweka msingi muhimu kwa mustakabali wa elimu na malezi ndani ya Jamiat Al-Mustafa (s) - Dar-es-salaam-Tanzania, huku wajumbe wakiahidi kuendelea kushirikiana kwa karibu katika kuboresha mwelekeo wa kielimu na kijamii kwa manufaa ya wanafunzi na jamii kwa ujumla.
Tunawapongeza waalimu waliowafundisha wasichana hawa wa Kiislamu kwa bidii na uaminifu, na pia Mkurugenzi Mkuu wa Taasisi ya Kimataifa ya Jamiatul Mustafa (s) - Tanzania, Hojjatul Wal Muslimin, Dr.Ali Taqavi aliyekuja na wazo hili muhimu na kulisimamia kwa hekima na juhudi kubwa.