Meya wa Tehran, Alireza Zakani, amesema kuwa wale wanaohusika na kuuawa kwa Kiongozi Mkuu wa Iran, Ayatullah Sayyid Ali Khamenei, watakabiliwa na hatua za kulipiza kisasi, akisema kuwa Rais wa Marekani Donald Trump "hatakuwa salama popote duniani."
Waandamanaji walibeba mabango na kuziba baadhi ya barabara wakitaka hatua za haraka za kimataifa kuchukuliwa. Baadaye maandamano hayo yalizingira mgahawa wa OWO, ambapo baadhi ya wabunge wa Uingereza waliripotiwa kuwa na kikao, kabla ya kumalizika kwa amani kufuatia kuwasili kwa Polisi.