Zaidi ya raia milioni 6.5 wa Honduras watapiga kura Jumapili hii kuamua kama mradi wa kisiasa wa mrengo wa kushoto wa Rais Xiomara Castro na mgombea wake, Rexy Moncada, utaendelea au la, au kama shinikizo la Donald Trump litaweza kumsaidia Nasry Asfura, mgombea wa mrengo wa kulia, kufanikisha ushindi.
Ofisi ya Habari ya Serikali ya Palestina katika Ukanda wa Gaza imelaani vikali kura ya veto iliyowekwa na Marekani dhidi ya azimio la Baraza la Usalama la Umoja wa Mataifa, na kuitaja kama ishara ya wazi ya uungaji mkono wa Washington kwa uhalifu unaotekelezwa na utawala wa Kizayuni. Taasisi hiyo imesisitiza kuwa hatua hiyo itaongeza mgogoro wa kibinadamu huko Gaza na kusababisha kuongezeka kwa mauaji ya raia wasio na hatia. Imeyataka jumuiya ya kimataifa kuchukua hatua za haraka na madhubuti ili kuokoa maisha ya watu wasiokuwa na hatia katika eneo hilo.