Wanazuoni hao walionya kuwa tabia kama hiyo hufungua mlango kwa wenye misimamo mikali wa dini nyingine kushambulia matakatifu ya watu wengine, na hata Huongeza uwezekano wa vitendo vya kulipiza kisasi, jambo ambalo jamii ya Marekani inaweza kuathirika nalo kwa kiwango kikubwa.
Shia na Mtazamo wao kwa Masahaba
Shia hawawatusi Masahaba wa Mtume (s.a.w.w), bali hukosoa matendo au maneno ya baadhi yao pale yanapopingana na mafundisho ya Uislamu na Qur’an Tukufu. Kukosoa kwao si kutokana na chuki, bali ni kutokana na ufuasi wa haki na uchambuzi wa kielimu.