"Tuepuke upepo mbaya unaosambazwa kwa chuki za kidini. Sisi Waislamu hatukatazwi kuishi kwa wema na wasiokuwa Waislamu. Maisha ya watu lazima yalindwe,” alisema Mufti.
Sheikh Dr.Alhad Mussa Salum amewahimiza Waumini wa Dar es Salaam na maeneo ya jirani kuhudhuria kwa wingi, akisisitiza kuwa mwaka huu Maulid itakuwa na vionjo vya pekee, ikiwa ni kumbukumbu ya kumsifu na kufuata nyayo za Mtume Muhammad (s.a.w).