Waziri wa Mambo ya Nje wa Iran, Abbas Araghchi, amekutana na mabalozi wa nchi za Amerika ya Kusini mjini Tehran na kusisitiza umuhimu wa kuimarisha ushirikiano kati ya Iran na mataifa hayo, huku mabalozi wa Uruguay na Brazil wakimzawadia jezi za timu zao za taifa kama ishara ya urafiki.
"Tuepuke upepo mbaya unaosambazwa kwa chuki za kidini. Sisi Waislamu hatukatazwi kuishi kwa wema na wasiokuwa Waislamu. Maisha ya watu lazima yalindwe,” alisema Mufti.
Sheikh Dr.Alhad Mussa Salum amewahimiza Waumini wa Dar es Salaam na maeneo ya jirani kuhudhuria kwa wingi, akisisitiza kuwa mwaka huu Maulid itakuwa na vionjo vya pekee, ikiwa ni kumbukumbu ya kumsifu na kufuata nyayo za Mtume Muhammad (s.a.w).