Ayatullah Haj Sayyid Javad Golpayegani, mtoto wa Marja’ al-Marhumu’ wa Shia aliyefariki, ameelezea baadhi ya vipengele vya maisha na umarja wa baba yake katika mkutano wa waandishi wa habari ulioandaliwa kwa heshima yake.
Akimkumbuka baba yake, alirejelea ndoto ya Ayatullah al-Uzma Golpayegani kuhusu msaada wa ghaib wa Imam Zaman (A.J.) kwa Chuo cha Dini cha Qom, akithibitisha kwamba huduma za shule na maktaba zinaendelea hata baada ya kifo chake.
Aidha, alikosoa hatua ya kuondolewa kwa usimamizi wa Hospitali ya Qom kutoka chini ya Bait al-Marja’iyya, akionyesha wasiwasi wake kuhusu athari za kiutawala na usimamizi wa hospitali hiyo.
Katika taarifa yake muhimu na ya kina, Katibu Mkuu wa Jukmuiya ya Kimataifa ya Ahlul Bayt (as) -ABNA - amelaani matusi na vitisho vya hivi karibuni dhidi ya Kiongozi Muadhamu wa Mapinduzi ya Kiislamu ya Iran na kushukuru misimamo yenye nuru ya viongozi na wasomi wakuu (Marajii) wa kidini duniani.