Masjid
-
Mada ya Ijumaa Masjidul Ghadir Kigogo Post: "Hijjah na Athari Zake Katika Malezi (ya Watoto na Jamii)"
Tarehe: Ijumaa, 30 Mei 2025. Mahali: Masjidul Ghadir, Kigogo Post – Dar-es-Salaam, Tanzania. Khatibu wa Swala ya Ijumaa: Maulana Sheikh Hemed Jalala. Mada ya Khutba ya Ijumaa: "Hijjah na Athari Zake Katika Malezi". Khutba hii iliangazia Nafasi ya Hijjah kama Shule ya Malezi ya kina, ikihimiza wazazi na jamii kwa ujumla kutumia mafundisho ya Hijjah kuwalea watoto katika misingi ya Utii, Ucha Mungu, Uvumilivu, Unyenyekevu na Umoja. Pia, iliweka msisitizo wa umuhimu wa Mwezi wa Dhilhijja katika historia ya Uislamu na fadhila za ibada ndani yake.
-
Tunajifunza nini baada ya Mwezi Mtukufu wa Ramadhan?
Aliyekuwa akifanya Ibada za Usiku ndani ya Ramadhani na mwendo wake ukabadilika na tabia zake kuwa nzuri ndani ya Ramadhan, basi aendelee kuwa na tabia nzuri hivyo hivyo hata baada ya Ramadhan. Na hii ni sehemu ya wito na funzo zuri toka kwa Mtume wetu Muhammad (s.a.w.w).
-
Kauli mbiu: Amani ya Palestina ni Amani ya Tanzania;
Majlis ya Siku ya Kupigwa Upanga Imam Ali (a.s), imefanyika katika Hawza ya Imam Sadiq (a.s), Kigogo, Dar-es-Salam, Tanzania
Maulana Sheikh Hemed Jalala: "Adui Ibn Muljim (laana iwe juu yake), aliyempiga Imam Ali (a.s) kwa upanga wenye sumu kali, alijua kuwa hawezi kupambana na Imam Ali (a.s) akiwa nje ya Msikiti, hivyo akaona mbinu aliyokuwa nayo ni kumuwinda akiwa katika ibada (swala), kwani awapo katika swala huwa mwili wake na hisia zake zinatoweka Duniani, na anazungumza na Mola wake Mtukufu kama vile hayupo Duniani".