Rais Dkt. Mwinyi pia ameswali Sala ya Ijumaa katika Msikiti wa 'Abdallah Rashid', ikiwa ni hatua inayotekeleza utaratibu wake wa kawaida wa kusali katika Misikiti mbalimbali nchini, kwa lengo la kuimarisha mshikamano wa kijamii na kudumisha mahusiano ya karibu kati ya Viongozi na Waumini.
Tarehe: Ijumaa, 30 Mei 2025. Mahali: Masjidul Ghadir, Kigogo Post – Dar-es-Salaam, Tanzania. Khatibu wa Swala ya Ijumaa: Maulana Sheikh Hemed Jalala. Mada ya Khutba ya Ijumaa: "Hijjah na Athari Zake Katika Malezi". Khutba hii iliangazia Nafasi ya Hijjah kama Shule ya Malezi ya kina, ikihimiza wazazi na jamii kwa ujumla kutumia mafundisho ya Hijjah kuwalea watoto katika misingi ya Utii, Ucha Mungu, Uvumilivu, Unyenyekevu na Umoja. Pia, iliweka msisitizo wa umuhimu wa Mwezi wa Dhilhijja katika historia ya Uislamu na fadhila za ibada ndani yake.