Rais wa Venezuela Nicolás Maduro amesema mbele ya mahakama ya New York kuwa yeye ni mfungwa wa vita, akisisitiza kuwa hana hatia na hakubali mashtaka yote yanayomkabili yeye na mkewe. Mahakama imeruhusu wawili hao kuwasiliana na ubalozi wa nchi yao, huku wakili wa Maduro akibainisha kuwa kwa sasa hawajaomba dhamana lakini wanaacha uwezekano huo wazi baadaye.
Utawala wa Kizayuni umetangaza kuwa umepokea mabaki ya mwili wa Itay Chen, mateka wa mwisho mwenye uraia wa pande mbili -Marekani na Israel- aliyekuwa akishikiliwa katika Ukanda wa Gaza.