Mhimili
-
Qalibaf: Mazishi ya Kihistoria ya Kiongozi Shahidi nchini Iraq Yalikuwa Tamko la Kulipiza Damu Yake
Spika wa Bunge la Jamhuri ya Kiislamu ya Iran, Mohammad Baqer Qalibaf, amesema mazishi ya kihistoria ya Kiongozi wa Mapinduzi ya Kiislamu aliyeuawa shahidi nchini Iraq hayakuwa tukio la maombolezo pekee, bali yalikuwa tamko la kuendeleza njia yake na kulipiza damu yake.
-
Mkuu wa Mahakama ya Iran: Tutatekeleza majukumu tuliyokabidhiwa kwa uaminifu na juhudi zote
Mkuu wa Idara ya Mahakama ya Iran, Hujjatul-Islam Gholam Hossein Mohseni Ejei, amesema ataelekeza uwezo wake wote katika kutekeleza majukumu aliyopewa baada ya kuteuliwa tena kuongoza mhimili huo.
-
Kamanda wa Makao Makuu ya Khatamul Al-Anbiya Ampongeza Mohseni-Ejei kwa Kuteuliwa Tena Kuongoza Mhimili wa Mahakama
Kamanda wa Makao Makuu ya Khatam al-Anbiya (s), Meja Jenerali Ali Abdollahi, amesema kutekeleza maelekezo ya Kiongozi wa Mapinduzi ya Kiislamu na kuzingatia matarajio ya Kiongozi Shahidi kutahakikisha mafanikio endelevu ya Mkuu wa Mhimili wa Mahakama wa Iran.
-
-
Qalibaf: Pakistan ni rafiki wa kweli katika nyakati zote
Spika wa Bunge la Iran ameandika kwenye ukurasa wake binafsi katika mitandao ya kijamii kuwa:“Kwa mwaliko maalumu wa Mheshimiwa Spika wa Bunge la Kitaifa la Pakistan, nimeelekea nchini humo. Kuimarisha uhusiano wa pande mbili kati ya mataifa haya mawili ndugu - hususan katika nyanja za ushirikiano wa kiuchumi na kiusalama - kutakuwa ndiyo mhimili mkuu wa ziara hii.”
-
Jeshi la Israel ladaiwa kumuua “Muhammad Akram Arabiyeh” mwanachama wa Kikosi cha Rizwan cha Hezbollah
Kwa mujibu wa vyanzo vya Kizayuni, katika kuendeleza uvamizi wake ndani ya ardhi ya Lebanon na mashambulizi dhidi ya wapiganaji wa muqawama, mwanachama wa Kikosi Maalumu cha Ridhwan cha Hezbollah ameuawa shahidi katika shambulizi la anga lililofanywa na Israel katika eneo la al-Qulay‘a, kusini mwa Lebanon.