Spika wa Bunge la Iran ameandika kwenye ukurasa wake binafsi katika mitandao ya kijamii kuwa:“Kwa mwaliko maalumu wa Mheshimiwa Spika wa Bunge la Kitaifa la Pakistan, nimeelekea nchini humo.
Kuimarisha uhusiano wa pande mbili kati ya mataifa haya mawili ndugu - hususan katika nyanja za ushirikiano wa kiuchumi na kiusalama - kutakuwa ndiyo mhimili mkuu wa ziara hii.”
Kwa mujibu wa vyanzo vya Kizayuni, katika kuendeleza uvamizi wake ndani ya ardhi ya Lebanon na mashambulizi dhidi ya wapiganaji wa muqawama, mwanachama wa Kikosi Maalumu cha Ridhwan cha Hezbollah ameuawa shahidi katika shambulizi la anga lililofanywa na Israel katika eneo la al-Qulay‘a, kusini mwa Lebanon.