Mojawapo ya malengo ya Mitume na Maimam (amani iwe juu yao), ni kusimamisha uadilifu na usawa katika jamii. Kwa mujibu wa Qur'an na hadithi za Maimamu, jamii haiwezi kusimama bila ya uongozi wa Imam Mwadilifu atakayeongoza masuala ya kidini na kijamii. Imam ni mlinzi wa sheria na mwongoza watu kuelekea haki na mafanikio.
Sheikh Athman Akbar alihimiza jamii ya Kiislamu kuiga nyayo za Imam Sajjad (a.s) kwa kuitumia dua kama silaha ya kiroho, kuimarisha subira katika majaribu, na kusimamia ukweli mbele ya dhulma ili kuendeleza ujumbe wa Karbala katika zama zote.