Rais wa Jamhuri ya Kiislamu ya Iran, Masoud Pezeshkian, amesema ushirikiano wa kimkakati kati ya Tehran na Moscow unaendelea kuimarika na kupanuka, akisisitiza dhamira ya kuendeleza mahusiano hayo kwa manufaa ya mataifa yote mawili.
Rais wa Ukraine, Volodymyr Zelensky, ameiweka wazi kuwa anatarajia kupokea jibu la Moscow leo Jumatano kuhusu rasimu mpya ya pendekezo la kumaliza vita, iliyokubaliwa awali kati ya Washington na Kyiv. Hata hivyo, Zelensky amesisitiza kuwa Ukraine haitaweza kukubali sharti lolote linalohusiana na kujiunga au kutokuwa mwanachama wa NATO, jambo ambalo Urusi ilikuwa imependekeza, akionyesha wazi kuwa suala hilo haliwezi kuwa kikwazo cha mazungumzo ya amani.