Mwanafikra wa Misri, Mustafa Mahmoud, aliwahi kuonya kuwa mataifa yanayoendelea hayapaswi kutegemea ahadi na mikataba ya mataifa makubwa kama dhamana ya usalama na ustawi wao, akisisitiza umuhimu wa kujitegemea kiuchumi, kulinda rasilimali za taifa na kudumisha umoja wa kitaifa ili kukabiliana na changamoto na maslahi ya kisiasa katika mfumo wa kimataifa.
Mwanafikra mashuhuri wa Algeria amesisitiza kuwa umoja wa Waislamu, kuacha misimamo ya chuki za kimadhehebu na kuunga mkono Iran kama ngome ya mbele ya kulinda Quds (Msikiti wa Al-Aqsa) na Umma wa Kiislamu ni jambo la lazima, na kwamba mataifa pamoja na wanazuoni wa Kiislamu wanapaswa kusimama bega kwa bega na Jamhuri ya Kiislamu ya Iran katika nyanja za vyombo vya habari, siasa, utamaduni na usalama.