Rais wa Shirika la Nishati ya Atomiki ya Iran katika hafla ya ufunguzi wa Kituo cha Mionzi kaskazini-magharibi mwa nchi, alieleza kwamba teknolojia ya nyuklia ni tasnia ya kisasa, na matumizi ya mionzi ni hatua muhimu katika kuboresha afya na usalama wa chakula nchini. Pia alisisitiza kuwa teknolojia hii inaweza kuleta baraka nyingi kwa wananchi wa Iran.
Kila Aya katika Aya za Qur’an ni chimbuko la mwangaza, muongozo na rahma, kwa hiyo mwenye kutaka mafanikio ya milele na kuokoka katika dunia yake, basi ni juu yake kushikamana na kitabu cha Mwenyeezi Mungu (s.w) usiku na mchana na kuzifanya Aya za Qur’an Tukufu kuwa mfano katika kumbukumbu zake na kituo cha fikra zake ili awe katika mwangaza wa Mwenyeezi Mungu (s.w).