Tangu kuingia madarakani, serikali ya Ahmed al-Shar‘a, anayejitambulisha kama rais wa Syria, imekuwa ikizidi kubana uhuru wa maoni na kujieleza, na imewakamata watu kadhaa, wakiwemo baadhi ya walio na ushawishi mkubwa katika mitandao ya kijamii.
Umoja wa Ulaya unakusudia kumuwekea vikwazo Abdulrahim Dagalo, Naibu Kamanda wa Kikosi cha Mwitikio wa Haraka (RSF) nchini Sudan, kwa tuhuma za ukiukaji wa haki za binadamu.