Salam
-
Iran Yalaani Vikali Shambulio la Kigaidi Kusini Magharibi mwa Pakistan
Msemaji wa Wizara ya Mambo ya Nje ya Iran, Ismail Baqaei, amelaani vikali shambulio la kigaidi lililotokea katika mji wa Khuzdar kusini magharibi mwa Pakistan, akitoa salamu za pole kwa familia za wahanga na kusisitiza umuhimu wa ushirikiano wa kikanda katika kupambana na ugaidi.
-
Ayatollah Dkt. Abbasi, kupitia ujumbe wake, amempa pole Hujjatul-Islam wal-Muslimin Sayyid Aref Naqavi kufuatia kufariki dunia kwa mke wake mpendwa
Ayatollah Dkt. Abbasi ametoa ujumbe wa rambirambi kwa Hujjatul-Islam wal-Muslimin Sayyid Aref Naqavi kufuatia kufariki dunia kwa mke wake, akimuomba Mwenyezi Mungu amrehemu marehemu na awajaalie wafiwa subira na malipo mema.
-
Salamu za Krismasi za Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Dkt. Samia Suluhu Hassan
Rais Dkt.Samia Suluhu Hassan: "Ninawatakia kheri ya Sikukuu ya Krismasi Wakristo na Watanzania wote. Mnaposafiri na kujumuika na ndugu, jamaa na marafiki katika maeneo mbalimbali ya nchi yetu, tusherehekee sikukuu hii kwa furaha, amani na upendo."
-
Salam za Rambirambi za Baraza la Maulamaa na Wenye Mamlaka wa Madhhebu ya Shia nchini Afghanistan Kufuatia Tetemeko la Ardhi Mashariki mwa Afghanistan
Baraza la Maulamaa na Watu Wenye Mamlaka wa Madhehebu ya Shia nchini Afghanistan, kupitia taarifa rasmi, limeeleza masikitiko na mshikamano wao na familia za waathirika wa tetemeko la ardhi lililotokea hivi karibuni katika mkoa wa Kunar, mashariki mwa Afghanistan, huku likisisitiza umoja wa kitaifa na hitajio la msaada wa haraka kwa waathirika.