Vyombo vya Habari vya Iran vimeripoti kuwa picha za satelaiti zinaonyesha shambulizi la usahihi lililosababisha kuharibiwa kwa hangar ya ndege za kivita katika Kambi ya Muwafaq Al-Salti nchini Jordan, ambako kuna wanajeshi wa Marekani.
Shirika la Anga za Juu la Iran limetangaza mipango mikubwa ya mwaka 2026, ikiwemo kuzindua satelaiti ya kwanza ya rada iliyotengenezwa nchini, kuendeleza mradi wa satelaiti 24 za “Shahid Soleimani” na kuharakisha maendeleo ya satelaiti za mawasiliano na uchunguzi wa ardhini.