Sunna
-
Andiko Kamili la Khutba ya Fadak ya Bibi Fātima Zahra (a.s) pamoja na tarjama yake
1. Mwanzo wa Khutba – Malalamiko kuhusu dhulma na msimamo wa watu Kisha hamkungoja hata kidogo ili moyo uliokuwa umejeruhiwa utulie, na hali ile ngumu iwe nyepesi. Bali mliongeza kuni kwenye moto, mkaufukuzia upepo ili uongezeke kuwaka. Mlikuwa tayari kuitikia mwito wa Shetani, mkijiandaa kuzima nuru angavu ya dini ya Mwenyezi Mungu, na kuondoa Sunna za Mtume Muhammad (s.a.w.w) aliyechaguliwa. Kwa kisingizio cha maslahi, mlikuwa mkila kijuujuu na kuficha nia zenu. Mlikuwa mkifanya njama nyuma ya vilima na miti dhidi ya familia yake na watoto wake. Na sisi tulipaswa kustahimili mambo haya yenye uchungu kama kisu chenye makali makali, au mkuki unaopenya tumboni.
-
Haj Mirza Baqer; Mweka Waqfu wa Maukufu Maarufu ya Fatimiyya huko Qom
Miongoni mwa maukufu (mambo yaliyowekwa wakfu) machache ya Qom yaliyosajiliwa kwa nia ya kuadhimisha maombolezo ya Bibi Fatima Zahra (a.s) na ambayo bado yanaendelea kutumika hadi leo, ni maukufu (yaliyowekwa na Haj Mirza Baqer katika miaka ya ishirini ya karne iliyopita.
-
Uchambuzi na Tathmini ya Thawabu za Ajabu na za Kipekee kwa Matendo Rahisi
Kuwepo kwa thawabu kubwa kwa baadhi ya matendo rahisi ni jambo lisilopingika, kwa sababu mizani ya Mwenyezi Mungu katika kutoa malipo haifanani na mizani ya kidunia.
-
Ni ipi kati ya ibara hizi mbili iliyo sahihi? "Kitabu cha Mwenyezi Mungu na Itrah wangu, Ahlul-Bayt wangu au Kitabu cha Mwenyezi Mungu na Sunna yangu"
Hadithi sahihi na iliyothibitishwa kutoka kwa Mtume Muhammad (s.a.w.w) ni yenye lafdhi hii isemayo: «وأهل بیتي» / "Na Ahlul-Bayt wangu”, ama riwaya ile ambayo imepachikwa lafdhi au neno «وسنّتي» / “Na Sunna yangu” badala ya lafdhi ya asili na sahihi isemayo: «وأهل بیتي» / "Na Ahlul-Bayt wangu”, riwaya hiyo ni batili kwa mtazamo wa sanadi ya upokezi wa Hadithi husika.
-
Ahkam za Kisheria kwa Mujibu Ahlul-Bayt (a.s):
Hukumu za Kisheria zitakazomfanya Mwanadamu afaulu Kesho Siku ya Kiyama
Hukumu za Kiislamu zinakutaka Muislamu Itikadi yako iwe ni Itikadi sahihi. Na Uislamu unatufndisha kuwa haijuzu kwa Muislamu yeyote kumfuata (Kumqalid) mtu kuhusiana na suala la Kiitikadi, kwa maana kwamba: Lolote linalohusiana na itikadi, inabidi Muislamu ulikubali na kuliitikadia kwa kutegemea dalili na uthibitisho madhubuti ima wa: Qur’an Tukufu, au Hadithi na Sunna za Mtume (Rehma na amani ziwe juu yake na Aali zake) na Riwaya mbalimbali za Maimam watoharifu (amani iwe juu yao), au uwe ni uthibitisho unaotokana na dalili za kiakili.
-
Vi[indi vya Tafsiri ya Qur’an Tukufu:
Tafsiri ya Aya ya Kwanza ya Surat Al-Maidah
Kwa kuwa "Hakika ya Waumini ni ndugu", basi Muislamu anatakiwa kuhakikisha kuwa anatimiza Haki ya ndugu yake Muislamu, na anatetea Haki yake kama Muislamu na kama ndugu yake.