Sunna
-
Swala ya Kuomba Mvua Yafanyika katika Masjid al-Haram
Maelfu ya waumini wakusanyika katika Masjid al-Haram mjini Mecca kuswali Swala ya Kuomba Mvua (Istisqa), wakimuomba Mwenyezi Mungu ateremshe rehema na mvua baada ya kipindi cha ukame.
-
Andiko Kamili la Khutba ya Fadak ya Bibi Fātima Zahra (a.s) pamoja na tarjama yake
1. Mwanzo wa Khutba – Malalamiko kuhusu dhulma na msimamo wa watu Kisha hamkungoja hata kidogo ili moyo uliokuwa umejeruhiwa utulie, na hali ile ngumu iwe nyepesi. Bali mliongeza kuni kwenye moto, mkaufukuzia upepo ili uongezeke kuwaka. Mlikuwa tayari kuitikia mwito wa Shetani, mkijiandaa kuzima nuru angavu ya dini ya Mwenyezi Mungu, na kuondoa Sunna za Mtume Muhammad (s.a.w.w) aliyechaguliwa. Kwa kisingizio cha maslahi, mlikuwa mkila kijuujuu na kuficha nia zenu. Mlikuwa mkifanya njama nyuma ya vilima na miti dhidi ya familia yake na watoto wake. Na sisi tulipaswa kustahimili mambo haya yenye uchungu kama kisu chenye makali makali, au mkuki unaopenya tumboni.
-
Haj Mirza Baqer; Mweka Waqfu wa Maukufu Maarufu ya Fatimiyya huko Qom
Miongoni mwa maukufu (mambo yaliyowekwa wakfu) machache ya Qom yaliyosajiliwa kwa nia ya kuadhimisha maombolezo ya Bibi Fatima Zahra (a.s) na ambayo bado yanaendelea kutumika hadi leo, ni maukufu (yaliyowekwa na Haj Mirza Baqer katika miaka ya ishirini ya karne iliyopita.
-
Uchambuzi na Tathmini ya Thawabu za Ajabu na za Kipekee kwa Matendo Rahisi
Kuwepo kwa thawabu kubwa kwa baadhi ya matendo rahisi ni jambo lisilopingika, kwa sababu mizani ya Mwenyezi Mungu katika kutoa malipo haifanani na mizani ya kidunia.