Sunna
-
Ni ipi kati ya ibara hizi mbili iliyo sahihi? "Kitabu cha Mwenyezi Mungu na Itrah wangu, Ahlul-Bayt wangu au Kitabu cha Mwenyezi Mungu na Sunna yangu"
Hadithi sahihi na iliyothibitishwa kutoka kwa Mtume Muhammad (s.a.w.w) ni yenye lafdhi hii isemayo: «وأهل بیتي» / "Na Ahlul-Bayt wangu”, ama riwaya ile ambayo imepachikwa lafdhi au neno «وسنّتي» / “Na Sunna yangu” badala ya lafdhi ya asili na sahihi isemayo: «وأهل بیتي» / "Na Ahlul-Bayt wangu”, riwaya hiyo ni batili kwa mtazamo wa sanadi ya upokezi wa Hadithi husika.
-
Ahkam za Kisheria kwa Mujibu Ahlul-Bayt (a.s):
Hukumu za Kisheria zitakazomfanya Mwanadamu afaulu Kesho Siku ya Kiyama
Hukumu za Kiislamu zinakutaka Muislamu Itikadi yako iwe ni Itikadi sahihi. Na Uislamu unatufndisha kuwa haijuzu kwa Muislamu yeyote kumfuata (Kumqalid) mtu kuhusiana na suala la Kiitikadi, kwa maana kwamba: Lolote linalohusiana na itikadi, inabidi Muislamu ulikubali na kuliitikadia kwa kutegemea dalili na uthibitisho madhubuti ima wa: Qur’an Tukufu, au Hadithi na Sunna za Mtume (Rehma na amani ziwe juu yake na Aali zake) na Riwaya mbalimbali za Maimam watoharifu (amani iwe juu yao), au uwe ni uthibitisho unaotokana na dalili za kiakili.
-
Vi[indi vya Tafsiri ya Qur’an Tukufu:
Tafsiri ya Aya ya Kwanza ya Surat Al-Maidah
Kwa kuwa "Hakika ya Waumini ni ndugu", basi Muislamu anatakiwa kuhakikisha kuwa anatimiza Haki ya ndugu yake Muislamu, na anatetea Haki yake kama Muislamu na kama ndugu yake.